Fahamu Kilimo Bora Cha Mdalasini - Cinnamon - KILIMO NA UFUGAJI

Latest

Karibu uweze kujifunza na kujipatia elimu kuhusiana na kilimo na ufugaji ambapo utajifunza mbinu bora za kilimo na ufugaji pia utajifunza dondoo mbalimbali na mbinu bora na za kisasa za ufugaji

Tuesday, October 24, 2017

Fahamu Kilimo Bora Cha Mdalasini - Cinnamon

 AINA
Mchanganyiko; za kienyeji (ndogo) na za kigeni ( kubwa)

HALI YA HEWA NA UDONGO

  • Mvua nyingi za kutosha 2000mm -2500mm kwa mwaka
  • Udongo wenye rutuba
  • Joto kwa wingi
  • Hewa yenye unyevunyevu


KUSIA MBEGU KWENYE VITALU

  • Mbegu hupatikana kwenye miti iliyokomaa
  • Sia mbegu kwenye kitalu zikiwa nusu sentimeta chini ya udongo
  • Baada ya kuchipua, mbegu huchukua miezi 6 hadi mwaka mmoja kufikia umri wa kupandikiza shambani
  • Panda miche wakati wa masika
  • Panda kwa nafasi ya 2m x2m. Nafasi hizi huwezesha miti kutoa machipukizi mengi. Nafasi kubwa hufanya miti kuwa na matawi mengi pia mashina hayanenepi wala kurefuka

 UTUNZAJI

  • Acha machipukizi kwenye shina
  • Toa matawi kwenye mashina ili kunenepesha mashina
  • Weka shamba katika hali ya safi
  • Zuia magonjwa kama.
  • Vinundu (galls)wanaosababishwa na utitiri na wadudu scales na mealbugs kwa kutumia dawa za sumu kama Selecron, Karate nk.


KUVUNA

  • Anza kuvuna miaka 3 baada ya kupanda
  • Mazao ya mdalasini ni maganda ya mashina ya miti
  • Kata shina la mti,na tenganisha maganda na mti kwa njia ya kumenya
  • Kuwa mwangalifu ili ganda litoke vizuri bila kupasukapasuka
  • Seli za nje ya ganda la mdalasini ni chungu hivyo ni vizuri ziondolewe kwa kukaruza kwa kisu
  • Kausha vizuri siyo kwenye jua kali Mavuno
  • 0.25 kg – 10kg maganda yaliyokaushwa kwa mti mmoja. Kiasi cha mazao hutegemea ukubwa na umri wa mti
  • Ubora wa mdalasini hushuka kulingana na umri wa mti. Mti wa umri mkubwa hutoa mganda yenye ubora wa chini

 MATUMIZI

  • Mdalasini baada ya kukaushwa ikiwa umesagwa au bila kusagwa hutumika kama:
  • Kiungo kwenye chakula na vitafunwa kama keki, mandazi,vitumbua
  • Vikolezo kwenye vinjwaji km. chai, kahawa
  • Dawa ya tumbo hasa wakati wa kuvimbiwa, kutoa hewa tumboni pia kuongeza hamu ya chakula
  • Dawa ya ngozi


JINSI YA KUTUMIA

  • kiungo kwenye chakula
  • Tumia maganda au saga magada yaliyokauka. Tumia ili kuongeza ladha kwenye vyakula kama pilau, ndizi, mchuzi nk 
  • Kutengenezea kinywaji
  • Weka vipanda vichache 2-3 (30gm) vya maganda kwenye kikombe ongeza maji yanayochemka, funika kwa dakika 15, ongeza vipande vya limao. Kunywa kila baada ya kula

MANUFAA

  • Miti hudumu shambani zaidi ya miaka 20. Miti huchipua na kutoa machipukizi mengine kila baada ya kuvuna
  • Gharama ndogo ya uzalishaji
  • Mazao yaweza kuhifadhiwa kwa muda mrefu
  • Magonjwa na wadudu ni kidogo
  • Rahisi kuchanganya na mazao mengine
  • Nguvu kidogo, kipato kikubwa.

No comments:

Post a Comment