UGONJWA SUGU WA MFUMO WA HEWA - KILIMO NA UFUGAJI

Latest

Karibu uweze kujifunza na kujipatia elimu kuhusiana na kilimo na ufugaji ambapo utajifunza mbinu bora za kilimo na ufugaji pia utajifunza dondoo mbalimbali na mbinu bora na za kisasa za ufugaji

Friday, May 26, 2017

UGONJWA SUGU WA MFUMO WA HEWA

                                 


 UGONJWA SUGU WA MFUMO WA HEWA.

 (Chronic Respiratory Disease-CRD)

Maelezo

Ni ugonjwa unaosababishwa na bakteria ambao hushambulia zaidi kuku na bata mzinga.

Jinsi Ugonjwa Unavyoenea

 Chanzo cha maambukizi ni maji na chakula kilichochafuliwa na kinyesi cha kuku wagonjwa na wenye
vimelea. Pia kupitia mfumo wa hewa kutoka ndege wagonjwa.

 Njia kuu ya kuenea kwa maambukizi ni kupitia mayai, hivyo maambukizi huendelea kutoka kizazi hadi
kizazi.

 Tahadhari: Wageni, wafanyakazi na magari yanaweza kusambaza ugonjwa kutoka shamba hadi shamba
au banda hadi banda

Dalili

Ugonjwa huu hushambulia zaidi mfumo wa hewa na hivyo kusababisha dalili zifuatazo:
 Kuku hukoroma
 Kuku hutoa makamasi
 Kuku wanakohoa kwa muda mrefu, wiki hadi miezi
 Kuvimba macho
 Kutingisha kichwa
 Vifo vya kuku vinaweza kufikia hadi asilimia 20

Uchunguzi wa Mzoga
 Athari kubwa za ugonjwa huu ni kwenye mfumo wa hewa, hivyo mabadiliko yanakuwa katika mfumo
mzima wa hewa.
 Kamasi nzito zenye usaha zilizotapakaa kwenye pua, koromeo, mapafu na vifuko vya hewa
Tiba
 Madawa aina ya sulfa na antibiotiki yanaweza kutumika kwa ajili ya tiba na kinga.

_Tylosin
_Lincomycin
    Nk
Pata ushauri wa Doct

KILIMO NA UFUGAJIINAWATAKIA UFUGAJI MWEMA.

Usisahau Ku download app ya blog hii play store.

AU BOFYA HAPA CHINI UPAKUE APP YETU


                     

No comments:

Post a Comment